Ad Code

Responsive Advertisement

HISTORIA YETU

 

HISTORIA YA KIKUNDI CHA ANGAZIA MEMA

1.0.       JINA LA KIKUNDI         :                       ANGAZIA MEMA

KUANZISHWA               :                       2012                                      

MAKAO MAKUU          :                       Kawe, Kinondoni Dar es Salaam TZ

Mawsiliano

SIMU                             :                  0689654599

BARUA PEPE                :                  zagragroup@outlook.com

P.O.BOX                      :                   31902

 

2.0 Mahali kikundi kinapatikana.

Kikundi kinapatikana Mtaa wa ukwamani. Mkabala na ofisi ya mtendaji wa kata ya kawe.Jilani kabisa na soko la kawe.

3.0      KUANZISHWA KWA KIKUNDI

Kikundi kilianzishwa Mwaka 2012 kwa jina la Tegemea Mema kama kikundi cha       kuweka na kukopa. mwaka 2018 kikundi kikasajiliwa chini ya halimashauri ya manispaa ya Kinondoni kwa jina la ANGAZIA MEMA, na kupewa hati ya kuandikishwa, kuwa kikundi cha ujasiriamali na maendeo katika nyanja ya kibiashara na elimu katika ngazi ya ujuzi. Hii ni  kuwezesha kikundi kufikia malengo yake. Kikundi hii cha angazia mema ni endelevu.

B. Malengo ya ANGAZIA MEMA

(i)   Inaunganisha jamii kua kama familia moja katika elimu ya ngazi ya ujuzi , kujengea Jamii mazoea ya kutumia elimu iliyopo kujiajiri na kujiingizia kipato ili kupunguza  wimbi la vijana tegemezi. 

(ii) kujiandaa na wakati ujao Kwa Kuanzisha Shughuli za Ujasiriamali ambazo zaweza kutoa Ajira na maendeleo kwa Jamii

(iii)                Kuanzisha miradi ya maendeleo yenye lengo la kuhakisha kikundi kina uwezo wa kutekeleza shughuli zake.

(iv)   kujikita katika Mpango wa Rasilimali za Biashara,Usimamizi wa Uhusiano wa Vijana, WANAWAKE na walemavu katika maendeo, Usimamizi wa Maudhui ya Biashara ,Miundombinu ya Biashara, Uchanganuzi wa Biashara na Mafunzo na Uwezeshaji.

 

4.0 NAMBA YA USAJILI

Kikundi Kimesajiriwa na idara ya maendeleo ya jamii ya Halmashahauri ya Wilaya ya Kinondoni kwa Nambari. KMC/GGR/10858


5. WANACHAMA

Kikundi cha angazia mema kina Wanachama wa jinsia zote ambapo idadi kubwa ya wanchama wake ni wanawake. idadi ya wanachama wake wote ni therasini kama taratibu za vikundi vya vicoba zinavyo eleza. Pia wanachama wa angazia mema ni watu walielimishwa vizuri na wakapata uelewa juu ya utunzaji na uendesha wa shughuli za kikundi kwa maendeleo ya familia zao na jamii kwa ujumla .

‘Kila mwanachama ni kiongozi katika nafasi yake.’’ hii ni kauli mbiu ya kuwajenga wanachama wake ili kuwa wakundumu na endelevu kuyaikia malengo yao ya kimaisha.

6. MAENDELEO YA KIKUNDI

Kikundi cha angazia mema kina maendeleo makubwa  yanayo endana na umri wa kikundi tangu kianzishwa kwake. Maendeleo ya kikundi ni kama iuatavyo.

1.   MIRADI.Kikundi kimefanikiwa kumiliki shamba la hekari 10 huko vigwaza wilaya ya chalinze ambalo ni kama mradi wa pamoja kama  mwanzo wa Biashara ya uuzaji aridhi(vinjwa na mashamba.

2.   MAPATO. Kikundi kinakusanya makadilio ya mapato ya ndini TZS Mil. 60,000,000 hadi Mil. 63,000,000/=kwa mwaka Tangu wanachama kuelimika.

3.   MIKOPO. Kikundi kina aina mbili ya Mikopo yaani Mkopo wa  Biashara na mkopo wa jamii, Mkopo wa biashara hutolewa kwa kutozwa Ziada ya mkopo (riba) mkopo wa Jamii hutolewa Basipo kutozwa riba.Kikundi kimefikia kutoa mkopo wa biashara wa TZS 18,000,000 na Kuendelea kwa mwanachama mmoja mmoja tangu mwaka 2018, na wanachama  wote ni wadaiwa. Namna ya utoji mikopo Soma katiba ya kikundi.

4.   GAWIO LA FAIDA. Kikundi kimefikia kutoa gawio la faida kiasi cha TZS 1,475,000 Kwa mwanchama aliye na umiliki wa hisa nyingi ambapo mwenye Umiliki wa hisa chache Hupata si chini ya kiwango TZS 300,000 Kwa mwaka, Hizi nitakwimu za mwaka 2019-2020.

5.   MISAADA. Kikundi kimetenga Tzs 500,000/=Kwa kila mwanachama kumhudumia katika majanga ya kila siku (ugonjwa,Misiba nk) kwa mwaka mzima. Pia kikundi kimefanikisha kumuwezesha kila mwanchama kuwa na bima ya afya.

6.   USHAWISHI. Kikundi kimfeanikiwa kuzalisha vikundi vingine vitano ambavyo bado ni vichanga. Kwa ajili ya kuinua jamii yote kutoka katika dimbwi la utegemezi.

7.   MALENGO ENDELEVU. Kikundi kina mikakati ya kumiliki biashara nyingi zikiwemo biashara ya usafirishaji na miradi  ya uwekezaji wa aridhi ya Pamoja. Pia tunamikakati ya kuinua Maisha ya mwanachama mmoja mmoja kuikia uchumi unaolidhisha

7.0.    PONGEZI

Kikundi hii kimeweza kusimama na kukua kwa muda wote kutokana na viongozi wanaojitole kwa kadri wawezavyo kupigania kikundi kwa muda wao wote na nguvu na kifikra. Pamoja na ushilikianao mkubwa wanao upata kutoka katika serikali na wanachama.

Post a Comment

0 Comments

Ad Code

Responsive Advertisement